Tabibu Tv

Tabibu Tv

EBOLA BBC NEWS

Wednesday, September 3, 2014

Mtindi husaidia kutibu shinikizo la damu


Mtindi unaorodheshwa kuwa ni miongoni mwa vyakula bora kutokana na kuwa na virutubisho vingi  vya aina mbalimbali ambavyo vina faida nyingi katika mwili wa mwanadamu .

Miongoni mwa virutubisho vinavyopatikana katika maziwa ya mgando (mtindi) ni pamoja na calcium, phosphorus, rhiboflavin (vitamin B12), potassium, iodine na vinginevyo.

Asilimia kubwa ya wanajamii wengi hupendelea kusindika kinywaji hiki kwa muda mrefu na kisha kukitumia, hususani jamii ya Wamasai na Kimang’ati, ambao huyaweka maziwa hayo kwenye kibuyu.

Mbali na kuwa virutubisho hivyo vinapatikana ndani ya maziwa ya mgando ambayo wengi tunayafahamu kama mtindi, pia hupatikana bakteria hai ambao ni muhimu kiafya katika mwili wa binadamu (probiotics).


Watafiti wamebaini kuwa bakteria wanaopatikana katika mtindi hurefusha maisha kwa wazee, ni kinga kubwa kwa kina mama kutokana na maambukizo ya magonjwa ya ukeni na hata hupelekea  kupunguza  kiwango kikubwa cha shinikizo la damu la juu (high blood pressure level), lakini pia husaidia  kupunguza uzito mkubwa na unene uliopitiliza.

Kama inavyojulikana, kiwango cha shinikizo la damu kikiwa juu huleta magonjwa kama mshtuko wa moyo na kiharusi. Tafiti hizo zinasema kuwa probiotics zinasaidia kudhibiti viwango vya insulin, lehemu  na glukosi mwilini visizidi.

Wataalam hao kupitia tafiti hizo wamesema kuwa  maziwa yamgando (mtindi) yameokoa maisha ya walio wengi baada ya tathimini kutoka kwa wagonjwa zaidi ya 540 waliosumbuliwa na tatizo la shinikizo la damu.

Pamoja na hayo, idadi kubwa ya wagonjwa waliotumia kinywaji hiki walifanikiwa kupona baada ya muda usiopungua wiki nane, hivyo inapendekezwa kutumia kinywaji hiki kama sehemu ya lishe yetu.


Makala nyingine nyingi nzuri zitakazokuelimisha kuhusu afya ya tiba za asili hupatikana kila siku ya Alhamis ndani ya gazeti la TABIBU kwa shilingi 500/= tu. Hakikisha hukosi nakala yako.

No comments:

Post a Comment