Tabibu Tv

Tabibu Tv

EBOLA BBC NEWS

Thursday, September 11, 2014

WHO: Tanzania inashika namba mbili kwa kujinyonga



Shirika la afya Duniani (WHO) hivi karibuni limetoa ripoti yake inayoainisha idadi ya watu wanaojiua duniani, huku hali ikionesha kuongezeka na kufikia kiwango cha kutisha zaidi, ambapo katika ripoti hiyo Tanzania imeonekana kushika nafasi ya mbili barani Afrika. 
 
Ripoti hiyo ilieleza kwamba Tanzania iko katika nafasi hiyo ya pili barani Afrika ikiwa na asilimia 24.9 ya vifo hivyo vya kukusudia.

Hata hivyo, Shirika hili limesema kuwa katika kila sekunde 40 mtu mmoja anajiua na hivyo kusema kuwa tatizo hilo ni la kiafya pia na linahitajika kushughulikiwa.

Utafiti huo uliohusisha nchi 172 duniani ulizitaja nchi za barani Afrika kuwa na idadi kubwa ya watu wanaojiua, ambapo nchi hizo ni pamoja na Msumbiji, Tanzania, Burundi, Sudan Kusini na Uganda. Na D.W

No comments:

Post a Comment