Tabibu Tv

Tabibu Tv

EBOLA BBC NEWS

Thursday, September 18, 2014

Mapishi pia ni miongoni mwa mambo ambayo hupatikana kupitia gazeti lako la kila Alhamisi la TABIBU. Huu ni mfano tu, lakini kwa uhondo zaidi hakikisha hupitwi na TABIBU kila wiki

Karibu tutengeneze mkate wa mbogamboga
Na Firdaws Alinus
Karibu tena mpenzi msomaji wa TABIBU, leo tunalo mapishi ya mkate wa mbogamboga. Chakula hiki tumezoea kukikuta hasa hotelini au kwenye sherehe na kwenye ndege, watu walio wengi huamini kwamba kuandaa chakula hiki nyumbani ni gharama sana. Chakula hiki kina faida kiafya katika mwili wa mwanadamu. 


Mahitaji
Mafuta ya mmea vijiko vitano
Vitunguu maji na swaum.
Pilipili mboga (hoho)
Karoti, zukini,
Kijiko kimoja cha chumvi.
Nyanya,
Hamira chenga, unga wa ngano,
Mayai 2
Sukari na maji au maziwa kikombe 1.

Jinsi ya kuandaa
Tengeneza donge la mkate kwa kuchekecha unga wa ngano pamoja na hamira, weka sukari, chumvi na mayai kisha ongeza maji na uanze kuchanganya changanya kwa kukanda kama chapati tengeneza madonge madogomadogo ns usukume donge moja kama chapati kwenye ubao na ikishakamilika kuwa kama chapati tandaza kwenye kontena ya silva yenye pembe 4 na uache kidogo kwa dakika 35 hadi 45.

Wakati unasubiri hizo dakika hizo kufika kaanga vitunguu maji na swaumu na uendelee kukaanga mpaka rangi ibadilike kuwa ya kahawia kisha weka pilipili nyanya, hoho, karoti, zukini, pasley pika kwa dakika 20 hadi 30 ikiwa tayari jaza rosti hiyo katika donge lililo tandazwa katika kontena ya silva kisha chukua donge lingine lililosukumwa kama chapatti na utandaze juu ya rosti iliyopo kwenye donge ifunge vizuri kwa madonge hayo ya ngano. 

Baada ya hatua hizo zote unaweza ukaoka kwa kutumia jiko la mkaa au oven ya umeme.

Faida za mkate wa mbogamboga.
Waisrael ni watumiaji wakubwa wa mkate wa aina hii na ni chakula ambacho hubadilisha sukari pia husaidia kufyonzwa kwa mafuta mwilini kwa sababu ya ‘chlorine’ na kuna kiasi kidogo ‘calcium’  pia huboresha neva na kuimarisha mifupa na meno pia tatizo la kutopata usingizi hudhibitiwa ukuaji wa mwili hujengwa na selenium na zink husaidia uyeyusho na kufyonza vitamin C.

Mpenzi msomaji hadi kufikia hapo tutakuwa tumehitimisha mapishi yetu ya leo, ni matumaini yangu kuwa umefurahia mapishi. Tukutane tena wiki ijayo kwa muendelezo wa mapishi. 

Kwa mawasiliano na huduma nyingine za kiafya kupima kwa computer mwili mzima, kutoa sumu mwilini, matibabu na ushauri wa chakula gani utumie na hutakiwi kutumia kulingana na afya yako. Pia kufundishwa uandaaji wa vyakula tiba fika kariakoo mtaa wa msimbazi jengo la klabu ya simba ghorofa ya tatu au piga simu namba Dar es Salaam ni 0755 093 418 na 0715 093 418 na Arusha ni 0656 540 570 na 0763 254 490. Au wasiliana nasi kupitiaa ukurasa wetu wa facebook kwa jina la febronia miracle food. Pia barua pepe ni miraclefoodfebronia@yahoo.com

No comments:

Post a Comment