Tabibu Tv

Tabibu Tv

EBOLA BBC NEWS

BURUDANI

EDSON: NAANDAA TAMASHA KUSAIDIA YATIMA

Na Kennedy Chaya

MSANII wa muziki wa Injili Edsoni Mwasabwite anatarajia kuandaa tamasha la kusaidia yatima mwezi Novemba. Tamsha hilo pia linatarajia kuwalenga wazee na watoto wanaoishi katika mazingira magumu ili waweze kujiona kama sehemu muhimu katika jamii.

Akizungumza na gazeti hili hivi karibuni jijini Dar es Salaam, Edson alisema ni kawaida yake kutoa shukrani na sadaka ya fungu la kumi kusadia watu wasiojiweza.

Edsoni anasema, “nafahamu machungu wayapatayo watoto yatima hivyo ni muhimu kuwafariji ili wasikate tamaa kwani ipo siku yao watakapofanikiwa kama ilivyo kwangu na wengine.”

Aliongeza kuwa ni muhimu jamii kusamianiana, kuheshimiana na kutambua kila mtu ana nafasi yake katika jamii, kwani masikini wa leo ni tajiri wa kesho.

Edson amepata umaarufu sana kupitia albamu yake ya kwanza ya ‘Ni Kwa Neema na Rehema’ na wimbo wenye jina hilo lililopendwa na watu wengi. Wimbo huo umetawala katika matamasha na sherehe za harusi nyingi hapa nchini.


Msanii huyo kwa sasa anaandaa video ya albamu yake ya pili, yenye jina la ‘Mungu Amenisaidia’.

MZEE YUSUPH: MFALME WA TAARAFU ASIYE NA MPINZANI
Na Kennedy Chaya
NYOTA wa muziki wa Taarab, Mzee Yusuf amesema kuwa muziki huo kwa sasa umekuwa maarufu kiasi cha kujizolea mashabiki wengi tofauti na zamani.

Akizungumza na TABIBU jijini Dar es Salaam alisema muziki wa Taarab wakati unaanza ulizoeleka kama ni muziki wa pwani, lakini kwa sasa ni muziki unaopendwa na watu wote.

Mzee Yusuph alisema, “pamoja na muziki huo kuwa maarufu, mimi naendelea kuwa mfalme wa muziki huo nikiwa sina mshindani wa kushika nafasi yangu. Wamejaribu wameshindwa.”

Mzee Yusuph ambaye pia ni Mkurungezi wa Jahazi Modern Taarab, alisema anajivunia mafanikio makubwa aliyopata katika muziki huo na ndiyo maana kwa sasa anafikiria kujenga misikiti kadhaa huku Chanika jijini Dar es Salaam kama sehemu ya shukrani zake kwa Mungu.

Nyota huyo kwa sasa anatamba na wimbo wake mpya wa ‘Mahaba Niue’ chini ya bendi yake ya Jahazi Modern Taarab, bendi aliyoanzisha tangu mwaka 2006.


DK. CHENI 'NIMEKUBALI KUOLEWA'

Na Kennedy Chaya, Dar
Mwigizaji mkongwe nchini Muhsin Awadh maarufu kama Dk. Cheni amesema, ile filamu yake ya “Nimekubali kKolewa” iloyozuiliwa na Bodi ya Filamu Tanzania (TFB) kwa kile kilichosemekana kuwa kukiuka maadili ya Kitanzania sasa iko huru kuingia sokoni.

Akizungumza na gazeti hili jijini Dar es Salaam hivi karibuni, Dk.Cheni alisema bodi hiyo ilimfungia filamu hiyo kwa madai ya kuwepo maudhui yanayoashiria ushoga, saura ambalo linapigwa vita na Serikali.

“Nilipewa sharti la kufanya marekebisho katika sehemu zote ambazo bodi hiyo iliona kuwa maadili ya Kitanzania yalikiukwa, nikasahihisha makosa hayo na sasa filamu hiyo imepitishwa. Hivyo muda wowote kuanzia sasa itakuwa ikisambazwa katika maeneo mbalimbali nchini,” alisema Dk.Cheni.

Aidha Dk. Cheni aliongeza kuwa baada filamu yake hiyo kuwa huru kuingia sokoni atahakikisha anashirikiana vizuri na wadau wanaosambaza filamu hiyo ili iweze kuwafikia mashabikai wake kote nchini.


Msanii huyo alifafanua kuwa kwa sasa hafikirii kufanya filamu nyingine mpaka aone matokeo ya filamu yake ya “Nimekubali Kuolewa.”

BEN PAUL: NIMEPATA TABU SANA KWENYE MAPENZI

Na Juma Diwani, Dar

Nyota wa muziki wa R&B Bongo, Benard Paul maarufu kama Ben Paul ameliambia TABIBU wakati wa mahojiano maalum kuwa yupo mapumzikoni mkoa wa Mwanza lakini anajiandaa kufunga mwaka kwa kufanya kazi kubwa na jamii ili kuonesha upendo.

Msanii huyo ambaye hivi karibuni alitamba na wimbo wake unaoitwa ‘Upendo’ ambao unaendelea kufanya vizuri katika redio na runinga mbalimbali nchini alisema kuwa ameamua kwenda kupumzika Mwanza kutokana na uzuri wa mji huo na kuutaja kuwa ni mji wa pili anaoupenda baada ya Arusha ingawaje yeye nyumbani ni Dodoma.

Ben Paul ni msanii ambaye nyimbo zake nyingi zimejikita kwenye mapenzi na nilipomhoji kwa nini anaimba kuhusu mapenzi sana kuliko kitu kingine alisema kuwa kila anachokiimba kimeshawahi kumtokea katika safari yake ya mapenzi.

“Kila nyimbo ninayoimba ya mapenzi inanihusu kwa sababu nimepitia mengi katika mapenzi,” alisema msanii huyo.


Hata hivyo, Ben Paul alisema kuwa mpaka hatua aliyofikia kwa sasa kimziki inatokana na sapoti kubwa kutoka kwa mashabiki wake na kusema kuwa hatowaangusha, hivyo  wazidi kumpa sapoti ya kutosha.

No comments:

Post a Comment