Tabibu Tv

Tabibu Tv

EBOLA BBC NEWS

Thursday, September 18, 2014

Hivi ndivyo komamanga linavyoweza kulinda afya yako






Dk. Febronia Kalongoti
Habari mpenzi msomaji wa blog yetu ya TABIBU, natumaini mzima wa afya. Bado tunaendelea kupeana mambo mengi mazuri ambayo pengine huyajui au unayajua kwa uchache.

Leo tunakuletea tunda la komamanga na faida zake mwilini.

Komamanga ni tunda lenye asili ya India na Persia kwa jina la kisayansi ni Punica Granatum, lakini lililetwa Marekani na wawekezaji wa Kihispania na kwa sasa limejulikana dunia nzima.

Tunda hili hustawi sana kipindi cha mwezi wa tisa na wapili, na huweza kushamiri sana katika hali ya hewa ya joto, lakini pia komamanga ni hodari katika kumudu hali ya ukame.

Kama hujawahi kula komamanga huwezi jua nini unakosa, lakini ukweli ni kwamba komamanga sio tunda tu bali ni chakula kilichojawa na afya ya vitamin, madini pamoja na virutubisho vingine vingi vinavyoweza kufanya miili yetu kuwa na afya na nguvu tele.

Tunda hili pia linajulikana kama ‘Granada’ au Tufaa la kichina (Chinese Apple), hali kadhalika tunda hili hufahamika zaidi kwa uzuri wa juisi yake,

Mkomamanga huweza kukua kwa urefu wa mita 5 hadi 8 na ina uzito wa gram 200, huku ikiwa na ‘calories’ za kutosha. Ambapo katika gram 100 komamanga huweza kutupatia kiasi cha 83 ‘calories,’ pia tunda hilo linaelezwa kutokuwa na ‘cholesterol’ wala mafuta.

Virutubisho vinavyopatika katika komamanga
Ina vitamin C kwa wingi
Vitamin B5
Vitamin A
Vitamin E
Madini kama Potassium na Iron
Mbegu zake ni chanzo kizuri cha nyuzi nyuzi ‘fiber’


 

Kazi zake mwilini
Unywaji wa juisi ya mbegu za komamanga utakupa dozi kamili ya kansa, pia husaidia mtiririko wa damu kwenda vizuri katika mishipa ya damu, ambayo husaidia presha ya damu na kupunguza hatari ya magonjwa ya moyo, shinikizo la damu na kiharusi.

Hulinda meno kuzuia kuoza na kuhuisha mfumo wa kinga mwilini kwa kuondoa vijidudu bakteria na maambukizi ya virusi ndani ya mwili, lakini pia husaidia kutibu madhaifu ya tumbo kama kuharisha, kutopata choo na maambukizi mbalimbali, matatizo sugu ya gesi tumboni hasa vidonda vya tumbo, hupunguza tindikali tumboni n.k

Matumizi
Hutumika kama tunda likiwa bichi
Hutumika kama juisi
Hutumika likiwa limepikwa.

Natumaini mpenzi msomaji utakuwa umepata kujua umuhimu wa tunda hili kiafya mwilini.

Kumbuka Miracle Food hutoa mafunzo ya kutengeneza maziwa ya soya, almond, mahindi machanga, karanga na dengu. Pia hutoa matibabu ya matatizo mbalimbali yanayosumbua mwili.

Kwa mawasiliano na huduma nyingine za kiafya na ushauri fika Kariakoo mtaa wa Msimbazi jengo la Klubu ya Simba ghorofa ya tatu au piga simu namba  0755 -093 418 na 0715 – 093 418, Facebook: febronia miracle food au Google: miracle food clinic & counseling au Email: miraclefoodfebronia@yahoo.com

Kwa makala nyingine nyingi kama hizi hakikisha, hupitwi na nakala yako ya gazeti la TABIBU kila  siku ya Alhamisi kwa shilingi 500/= tu.


No comments:

Post a Comment