Tabibu Tv

Tabibu Tv

EBOLA BBC NEWS

Thursday, September 11, 2014

Viongozi Liberia walia na Ebola



Wataalam  wa afya wakivuta pumzi baada ya kutoa huduma kwa wagonjwa.
Waziri wa Ulinzi wa Liberia ameonya kuwa Ebola inatishia kuwepo kwa taifa hilo wakati virusi hivyo hatari vikisambaa mithiri ya “moto wa kichakani”. Huku Shirika la Afya Duniani (WHO) likiarifu kuongezeka kwa idadi ya vifo.

Hata hivyo, taarifa hizi zinafuatiwa na baada ya kutabiriwa kuwa maambukizi ya ugonjwa huo yatafikia kiwango cha juu kote Afrika Magharibi, Aidha WHO imeeleza kuwa Liberia ambayo imeshuhudia nusu ya jumla ya idadi ya vifo vilivyoripotiwa na huenda ikatarajia kupunguza tu kwa  usambaaji wa virusi hivyo, na wala siyo kuzuia.

Naye Waziri wa Ulinzi wa Liberia Brownie Samukai aliuambia mkutano wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuwa ugonjwa wa ebola unasambaa kwa kasi kama moto wa kichakani, huku ukikiteketeza kila kitu njiani mwake.

WHO imesema idadi ya vifo vya ebola imeongezeka hadi kufikia 2,296 kati ya visa vya maambukizi 4,293 nchini Liberia, Sierra Leone, Guinea na Nigeria kufikia Septemba 6. Takribani nusu ya maambukizi yote yalitokea katika kipindi cha siku 21 zilizopita.

Aidha, Mkuu wa Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Liberia, Karen Landgren naye alisema kuwa ugonjwa huo unasambaa nchini humo ''Bila huruma''.

Takwimu za hivi karibuni za WHO zinaonesha kuwapo kwa usambaaji wa kiholela wa ugonjwa huo na hali ikionesha kuwa ugonjwa huo hujipenyeza katika jamii zilizojaa watu bila vifaa maalum vya matibabu na zinazokosa kampeni za uhamasisho wa umma kuhusiana na mlipuko huo.

Wakati hayo yakiendelea Mkuu wa Kitengo cha Magonjwa wa WHO Sylvie Briand alisema lengo la sasa nchini Senegal na Nigeria ni kuhakikisha wanazuia kabisa maambukizi ya ugonjwa huo. NA. DW.

No comments:

Post a Comment