Tabibu Tv

Tabibu Tv

EBOLA BBC NEWS

Wednesday, September 3, 2014

Njia za kuepuka virusi hatari vya Ebola



Ebola ni mojawapo ya virusi hatari zaidi ulimwenguni, lakini ugonjwa huu hauambukizwi kupitia hewa, hivyo basi huwezi kuambukizwa ebola kama homa ya kawaida.

Madaktari wanasema kuepuka Ebola ni rahisi sana iwapo mtu atafuata tahadhari hizi muhimu zaidi:

1. Nawa mikono kwa sabuni na maji
Nawa mikono kila baada ya shughuli yoyote, hakikisha unatumia sabuni na maji safi na utumie taulo kujikausha. Ingawaje jambo hili linaweza kuwa gumu kwa wanaoishi kwenye makazi duni, na walio vijijini ambako maji safi hayapatikani kirahisi, lakini ni mbinu iliyothibitishwa kuweza kuua virusi vya ebola.


Pia wataalam wanashauri kusalimiana kwa mikono kuepukwa kwa ujumla.
Dk Unnis Krishnan wa Plan International aliarifu BBC, kuwa ebola husambazwa haraka watu wanapowasiliana ana kwa ana na maji maji ya kimwili ya waliougua. Hivyo ni vizuri kutumia njia nyingine za kujuliana hali.

2. Hakuna kugusana
Iwapo unashuku kuwa mtu ana ebola, usimguse. Ingawaje inaweza kuonekana kuwa si maadili mema unapoona unaowapenda wakihisi uchungu na unataka kuwakumbatia na kuwahudumia, lakini haiwezekani.

3. Epuka miili ya wafu
Iwapo unadhani mtu amefariki baada ya kuugua ebola, usiguse mwili wao, hata kama ni mila au desturi ya maziko. Hii ni hatari kwa sababu baada ya mtu anapofariki bado huweza kuambukizwa ebola kutoka kwa miili yao kwani bado inatoa maji maji ya mwili, ambayo huweza kuwa hatari zaidi.Ni vyema kufanya mipango ya kupata timu ya magwiji kushughulikia mwili huo haraka iwezekanavyo kwani ni hatari kuacha mwili wa mfu kwa muda mrefu katika eneo la makazi.


4. Usile nyama ya porini
Epuka kuwinda, kugusa, au kula nyama ya porini, kwa mfano popo, nyani na sokwe, kwani wanasayansi wanaamini kuwa hiyo ndiyo chanzo cha maambukizi kwa binadamu.



Pia wataalam wanashauri hata kama mnyama fulani wa porini huliwa katika eneo lenu na nyama yake ni tamu ni vyema kuepuka myama huyo kwani nyama yake au damu huweza kuwa na virusi hivyo. Hakikisha vyakula vyote vinapikwa inavyostahili.

5. Usiwe na hofu
Kueneza uvumi huongeza hofu. Usiogope wafanyakazi wa huduma za afya, pia usiamini matibabu ya kiasili ambayo hayajathibitishwa kutoa afueni, kwani suala hilo limechangia sana ongezeko la kuenea kwa virusi vya Ebola katika nchi zilizoathirika.
Mtu huweza kupata maambukizi ya ugonjwa huu endapo utagusa maji maji ya kimwili- mkojo na kinyesi, matapishi, kamasi, mate, machozi, na mbegu za kiume na majimaji ya uke- vyote huweza kueneza ebola endapo mhusika atakuwa ameathirika na ugonjwa huo.


Dalili za mtu aliyeugua ni joto mwilini, maumivu ya misuli na viungo, vidonda kooni, kuumwa na kichwa, na uchovu, kufuatiwa na kichefuchefu, kutapika na kuharisha, ambapo mtu huweza kutoa damu pia. Ebola bado haina tiba sasa. Na BBC

No comments:

Post a Comment