Tabibu Tv

Tabibu Tv

EBOLA BBC NEWS

Sunday, August 10, 2014

Tiba asilia ya kisukari



Baada ya Alhamisi ya Julai 7 blog yako ya TABIBU kukuletea makala maalum iliyokuwa ikihusu ugonjwa wa kisukari, ambapo ulipata kufahamu aina za ugonjwa huo pamoja na visababishi vyake na dalili pia, sasa leo tunakuletea namna ambavyo tiba asilia inavyoweza kusaidia katika kutibu ugonjwa huo pamoja na mashuhuda waliozungumza na TABIBU Endelea sasa…. 
  
Mashuhuda waliopona kwa tiba asilia
Kupitia gazeti letu la TABIBU ambalo hupatikani mtaani kila siku ya Alhamisi lilifanikiwa kukutana na Tausi Miraji, ambaye ni mkazi wa Bagamoyo eneo la Mwanakalenge block P. Anasema mwaka 2009 alianza kujisikia mwili ukimuuma sana na alikuwa anakunywa maji mengi na kukojoa mara kwa mara, mwili ulikuwa na ganzi, mguu ulivimba na ulikuja kupasuka wenyewe tu, lakini alikuwa akibanwa na kiu.

Mara baada ya kuona dalili hizo anasema alilazimika kwenda kupima kisukari na aligundulika kweli alikuwa na kisukari, ambapo ilikua ni kiwango cha 33 na alipatiwa dawa, ingawaje anakiri kuwa dawa hizo zilikuwa zikimsaidia kutuliza maumivu. Lakini kwa muda wote huo, anasema alikuwa akiendelea kutafuta dawa za asili kwa ajili ya tatizo hilo ndipo siku mmoja mme wake alisoma gazeti hili na kusoma habari ya Dk. Mohamed Mkweli, ambaye aliainisha kutibu magonjwa mbalimbali hususani yale sugu.

 “Mme wangu siku moja alienda Dar es Salaam na kumtafuta daktari huyo na kisha aliniletea dawa za Dk. Mkweli na nikaanza kutumia, lakini ilinichukua miezi 6 kuanza kupata nafuu,ikiwa ni pamoja na kiu ya maji kukata, pamoja choo kidogo nilikuwa nikipata kama kawaida hata kusafiri safari ya mbali kwa sasa naweza,” alisema Bi Tausi.
 
Aidha, anaendelea kusema kuwa dawa hiyo ya daktari huyo ilikuwa ni ya rangi kama ya kijani ikiwa katika mfumo wa maji na inaitwa ‘Special 2.’ Lakini  pia, alipewa dawa ya kuchua ambayo anasema ilimsaidia sana kutuliza ganzi na  maumivu aliyokuwa nayo na hatimaye kiwango chake kilishuka hadi kufikia 5.

“Dawa za Mkweli mimi naamini zinasaidia, maana mimi nilitakiwa kukatwa mguu hospitalini kwa sababu ya kisukari, lakini nashukuru sana baada ya dawa za daktari huyo, kidonda changu kilipona na hadi sasa naendelea vizuri kabisa,” alisema Tausi.

Pamoja na hayo, aliongeza kuwa, “kwa sababu vidonge vya hospitalini unapomeza huwa  vinakwenda kunyamazisha tu na ikiamua kuanza  inaanza tena, Kwa sababu mimi wakati sijatumia dawa za Dk. Mkweli hii mifupa ilikuwa inaniuma vibaya sana, lakini ni vizuri watu wasiache kunywa dawa za hospitalini lakini wajaribu kutumia na dawa za asili pengine zinaweza kuwasaidia kama ilivyonisaidia mimi”.

Naye mme wa Bi Tausi, Bw. Kilagu Miraji anasema hata yeye hakuamini kama mguu wa mke wake ungepona na sukari ingeshuka na alikuwa anaamini kuwa mguu ungekatwa tu, lakini anasema baada ya dawa za asili kutoka kwa Dk. Mkweli, mguu huo ulipona na hata sasa madaktari wake wa hospitalini wanashangaa kuona mama huyo kapona kidonda hicho pamoja na sukari yake kushuka.

 Tiba asilia
TABIBU lilimtafuta Dk Mohamed Mkweli, anayemiliki kituo cha magonjwa sugu  kiitwacho Afya Bora, yeye anasema kweli Bi Tausi alikuwa ni mgonjwa wake na alianza kumtibu akiwa na kiwango cha sukari 33.

Nafarijika sana kusikia wagonjwa wanaotumia tiba zangu wanendelea vizuri na baadhi wamekuwa wakishuhudia kwa watu wengine. Kikubwa mimi napenda kuwasihi Watanzania kuendelea kuziamini tiba hizi za asilia zitokanazo na mimea, kwani ni nzuri na hazina kemikali kabisa na mfano mzuri ni dawa yangu hiyo ya ‘Special 2,’ ambayo imewasaidia wengi hadi sasa na jambo zuri zaidi dawa hii imepitishwa na mkemia mkuu, kwa hiyo si ya kubabaisha kabisa,” alisema Dk. Mkweli.

“Kwa mfano, kama Tausi, yeye  nilipoanza kumpatia dawa zangu kiwango chake cha sukari kilikuwa ni 33, lakini hivi baada ya kutumia hii ‘Special 2’ hivi karibuni amekwenda kupima ananiambia imeshuka hadi kufikia 5. Kwa hiyo utaona kuwa anaendelea vizuri na dawa imeonekana kumsaidia,” alisema Dk. Mkweli.

Hata hivyo, Dk. Mkweli anasema kuwa anashukuru kwa ushirikiano unaotolewa kwa Serikali kuhusu tiba asilia ingawaje anasema jitihada zaidi bado zinahitajika katika kuhakikisha tiba hizo zinakuwa ni mkombozi wa magonjwa sugu hapa nchini.

Sambamba na hayo, Dk. Mkweli anasema kwa sasa kupitia kituo chake hicho anaendesha kampeni ya kuangamiza magonjwa yote sugu yanayoaminika hayatibiki. Huku akiyataja baadhi ya magonjwa wanayotibu kwa sasa kuwa ni kisukari, shinikizo la damu (BP), matatizo ya figo, moyo mpana, kifafa, pumu na matatizo ya kina mama n.k. 

Dk. Mkweli anakiri kuwa changamoto kubwa waliyonayo kwa sasa ni katika kutibu UKIMWI na saratani ya muda mrefu ambayo bado wanatafutia tiba yake.

Hata hivyo, Dk. Mkweli anasema kwamba ana mpango wa kutoa ofa kwa viongozi wa Serikali ili na wao wajue tiba asili imefikia wapi na kwa kiasi gani inasaidia kutibu magonjwa sugu.

“Mimi baadaye nitatoa ofa kwa viongozi wa Serikali wa Tanzania bara na Zanzibar wenye tatizo la presha ili nao waje tuwatibu kwa gharama zetu ili waje wadhibitishe kuwa kweli tunatibu na wajue tumefikia wapi maana inawezekana. Hawajui tiba asili tumefikia 
 wapi,” alisema Dk. Mkweli.
 
Ni vyema ikafahamika kuwa mgonjwa wa kisukari anaweza kupata afueni kupitia vyakula, vidonge na insulini. Vyote hivi huweza kumsaidia mgonjwa kushusha kiwango cha sukari katika damu. Ingawaje matumizi ya vidonge na sindano husaidia kumtuliza mgonjwa na si kuponesha na pindi mgonjwa anapoacha kutilia mkazo katika matumizi ya tiba au kuacha kutumia dawa, ugonjwa hurudi tena. Hivyo ni vyema kuzingatia ushauri wa wataalam wa afya muda wote.
Usikose gazeti lako la TABIBU kila Alhamisi mtaani ili uweze kufahamu habari nyingi pamoja na makala za afya kwa gharama ya shilingi 500/= tu.

No comments:

Post a Comment