Tabibu Tv

Tabibu Tv

EBOLA BBC NEWS

Friday, August 8, 2014

Kumbe kisukari kinatibika na kuisha kabisa

  •  Daktari ajitokeza, asema anayo tiba asilia
  •    Ajinadi kutoa ofa kwa viongozi wa kitaifa kuwatibu bure
  • Mashuhuda waliopona wajitokeza 
Ugonjwa wa kisukari hujitokeza wakati ambapo kongosho hushindwa kuzalisha insulini ya kutosha au wakati mwili unaposhindwa kutumia insulini inayozalishwa kwa ufanisi. Insulini ni homoni inayosimamai kiwango cha sukari katika damu. 

Kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani (WHO), takwimu zinaonesha kuwa mnamo mwaka 2010 zaidi ya asilimia 80 ya vifo vya ugonjwa wa kisukari vimekuwa vikitokea katika nchi za kipato cha chini na cha kati, huku wataalam wakisema kuwa, ifikapo mwaka 2030 idadi hiyo itaongezeka maradufu.

Sababu inayopelekea ugonjwa huu ni pamoja na mitindo ya maisha isiyofaa hususani maisha ya kisasa hasa kwa waishio maeneo ya mijini. Mitindo hiyo isiyofaa ni pamoja na aina ya vyakula vinavyoliwa, unywaji pombe na uvutaji sigara uliokithiri pamoja na kutofanya mazoezi ya mwili.

Inaelezwa kuwa mwaka 2004, watu  milioni 347 duniani kote walikuwa na kisukari, huku wastani wa watu milioni 3.4 walipoteza maisha kutokana na ugonjwa wa huo.
Ugonjwa wa kisukari hutokea pale tezi kongosho (pancrease) inaposhindwa kutengeneza homoni au kichocheo aina ya insulini au mwili unaposhindwa kutumia vizuri kichocheo hicho cha insulini na kusababisha kuongezeka kwa kiwango cha sukari kwenye damu au kitaalam ‘hyperglycemia’.

Insulini ni kichocheo au homoni inayotengenezwa na kongosho ili kudhibiti sukari katika damu. Aidha, ugonjwa wa kisukari unaweza kusababisha kuwa na kiwango kidogo cha insulini mwilini au mwili kutosikia kichocheo hicho au yote mawili.

Ugonjwa huu huwaathiri watu wengi hata hapa nchini kwa sasa, huku wengi wakionekana kujigundua na ugonjwa huu mara tu wanapoanza kuona dalili  kuu  za kisukari, ambapo wengi huchelewa sana kugundua. (Look for Tanzania statistics)

Aina za kisukari
Aina ya kwanza ya kisukari (Type 1 - Diabetes Mellitus). Hii ni aina ya ambayo huwaathiri zaidi watoto na vijana. Aina hii hujitokeza pale ambapo seli maalum zinazotengeneza homoni ya insulin zinakuwa zimekosekana katika tezi kongosho au kuharibika kutokana na sababu yoyote ile, na hivyo kusababisha ukosefu kabisa au upungufu wa kichocheo hicho kwenye damu.

Mambo yanayoweza kusababisha uharibifu wa seli hizo katika tezi kongosho ni pamoja na kushambuliwa tezi kongosho kunakoweza kutokana na magonjwa ya kinga ya mwili ya mtu mwenyewe (autoimmune diseases) au kushambuliwa na vyanzo visivyojulikana.
Wagonjwa wa aina hii ya kisukari huhitaji kupewa dawa za insulini kwa njia ya sindano au pampu kila siku za maisha yao ili waweze kuishi. Kwa sababu hiyo,aina hii ya kisukari huitwa pia kisukari kinachotegemea insulini (Insulin Dependent Diabetes Mellitus) (IDDM). 

Aina nyingine ya kisukari ni kisukari aina ya pili (Type 2 - Diabetes Mellitus). Hii ni aina ya kisukari inayotokea zaidi ukubwani. Aina hii ya kisukari husababishwa na kupunguza utendaji kazi wa homoni ya insulin au seli kushindwa kutumia insulini ipasavyo. Hali hii mara nyingi husababishwa na unene uliopitiliza yaani ‘obesity,’ au hali ya kutoushughulisha kabisa mwili.

Katika aina hii ya kisukari, insulini huzalishwa kwa kiwango cha kutosha, isipokuwa tatizo hujitokeza katika suala la ufanisi na utendaji kazi wake na hii inamaanisha kwamba wagonjwa wa aina hii ya kisukari huwa hawahitaji kupewa insulin kwa njia ya sindano. Aina hii hujulikana pia kama kisukari kisichotegemea insulin (Non-Insulin Dependent Diabetes Mellitus).

Aidha, mbali na aina hizo mbili pia kuna aina ya tatu, ambayo ni kisukari cha mimba (Gestational Diabetes Mellitus). Aina hii hutokea pale kunapokuwa na ongezeko la kiwango cha sukari katika damu (hyperglycemia) wakati wa ujauzito.

Aina hii ya kisukari huathiri karibu asilimia 2 hadi 5 ya mama wajawazito wote, ingawa wengi wao hupata nafuu na kupona kabisa mara tu baada ya kujifungua. Hata hivyo, wajawazito ambao hupata aina hii ya kisukari huweza kuendelea kuwa na ugonjwa huo hata baada ya ujauzito na hatimaye kuwa na aina ya pili ya kisukari maishani.

Visababishi vya kisukari
·        Matumizi ya sukari nyingi na vyakula vya mafuta
·        Kurithi kutoka kwa wazazi
·        Unywaji wa pombe wa kupindukia
·        Kutofanya mazoezi
·        Anasa na starehe na mtindo wa maisha usiofaa
·        Kula vyakula vilivyotengenezwa kwa kuongezewa sukari, hasa vyakula vya viwandani (processed foods) n.k.
Dalili za kisukari
Kukojoa mara kwa mara, mgonjwa kuhisi kiu kali na kunywa maji kwa kiwango cha kupitiliza, mgonjwa kuhisi njaa na kula mara kwa mara, kuchoka haraka, mgonjwa kuwa na hasira, kupungua uwezo wa kufikiri pamoja na kusikia njaa n.k.

Mbali na dalili hizo, mgonjwa pia huweza kupata madhara ya muda mrefu, ambayo ni pamoja na kupata mtoto wa jicho na upofu, magonjwa ya figo, kupata magonjwa ya kinywa na kung’oka kwa meno, mwili kufa ganzi na kupoteza hisia hasa mikononi na miguuni, vidonda kutopona upesi na hatari ya kukatwa mguu.  Hata hivyo, madhara haya ya muda mrefu huweza kuzuilika endapo mgonjwa atafuata masharti ya wataalam wa afya hasa kuhusu chakula na mazoezi na maelekezo ya utumiaji sahihi wa dawa au insulini. 

Pia kuna hatari zaidi ya watu wanopatwa na kisukari kupatwa na magonjwa ya moyo, kiharusi, kuharibika kwa kibofu cha mkojo, shinikizo la juu la damu sambamba na ugonjwa wa fangasi.

Baada ya kufahamu hayo kuhusiana na ugonjwa huu wa kisukari, blog ya gazeti hili la tabibu jumamosi hii itakuletea mashuda waliopona pamoja na namna tiba asili inavyotibu na kumaliza kisukari. Hakikisha hukosi muendelezo wa makala hii.
Gazeti lako la TABIBU wiki hii lipo mitaani na unaweza kujipatia nakala yako kwa shilingi 500/= kila Alhamisi.

No comments:

Post a Comment