Tabibu Tv

Tabibu Tv

EBOLA BBC NEWS

Thursday, August 7, 2014

NAMNA MIILI YETU INAVYOPOKEA SUMU


Karibu mpenzi msomaji wetu wa blog ya gazeti la TABIBU katika safu hii ya kutoka Miracle Food Clinic. Ambayo hupatikana ndani ya gazeti letu kila wiki Alhamisi, matumaini yangu u mzima wa afya tele.

Kuna vyakula vingi sana ambavyo vinaonekana kuvutia na kuwa na ladha nzuri mdomoni, lakini vita kubwa hufanyika wakati wa uyeyusho na katika ufanyaji kazi mwilini. Kwa mfano, mchanganyiko wa chumvi na kachumbari (salad) sio mzuri kiafya japokuwa una ladha nzuri, chumvi hufanya kazi ya kufyonza maji ambayo huondoka na virutubisho vyote unavyotegemea kuvipata kutoka kwenye kachumbari hiyo, hivyo kachumbari hubaki kuwa haina kazi mwilini.

Pia mpenzi msomaji unashauriwa kuepuka kuchanganya matunda machachu na matamu. Hii kwa ni sababu matunda machachu hupunguza kasi ya uyeyusho wa haraka wa sukari ya matunda matamu na kupelekea matunda matamu kuchacha.

Unaweza kujiuliza mbona vyakula hivi vinavyosemekana kuwa mchanganyiko wake ni hatari tumekuwa tukila kwa takribani maisha yetu yote bila athari? Jibu ni kwamba athari iletwayo na sumu ya vyakula, madawa, hewa na nyinginezo hutofautiana katika kutoa matokeo na kukujulisha kuwa unasumbuliwa na tatizo fulani. Hata hivyo, kumekuwa na magonjwa mengi makubwa yanayosumbua watu wengi huku wakijiuliza wamepata wapi athari hizo, kumbe ni mfumo uliojiwekea kwa kipindi kirefu na sasa ndio matokeo yake.

Tukiangalia mchanganyiko mwingine, tunakutana na kipengele cha vinywaji na vyakula vigumu,mfano chai, kahawa, pombe na vinywaji laini ukichanganya na chakula kigumu, mfano wa kitafunio, husababisha matatizo katika uyeyusho.
 

Pia epuka kula vyakula vya mafuta na protini. Miongoni mwa vyakula vinavyopasa kuliwa peke yake ni maziwa, tikiti (huyeyuka kwa urahisi kuliko tunda lolote na ni rahisi kuchacha). Kuhusu vinywaji, ni kama sheria ilivyo, vinywaji havipaswi kuliwa na vyakula vigumu. Kinywaji kina tabia ya kupita kwa kasi mpaka tumboni (utumbo) na kuchukua vimeng’enyo vyote vya uyeyusho ambapo kitendo hicho huzuia uyeyusho kufanya kazi nyingine.

Matunda yanatakiwa yaliwe peke yake tena nusu saa kabla ya mlo kamili. Sukari pia huchukua ratiba sawa na matunda.

Baada ya kueleza hayo, mpenzi msomaji sasa tuangalie unawezaje kuboresha uyeyusho (tumboni).

·      Kula pindi unapohisi njaa, mwili unaweza kuvumilia matokeo yoyote ya hatari hata kama mchanganyiko wa chakula sio mzuri endapo tu kama una njaa.
·      Fanya mazoezi mepesi kwa afya ya tumbo lako na uyeyusho kwa ujumla.
·      Kula chakula cha aina moja au kiasi kwa wakati. Vyakula vya aina nyingi huleta shida katika tumbo na uyeyusho kwa ujumla wakati tumbo linaweza kuvumilia aina moja ya chakula au chakula kiasi. Hivyo basi, ulaji wa vyakula vingi huvifanya visubiriane katika uyeyusho na hicho sio kitu sahihi kiafya.
Kuwa na tabia ya kula vyakula vibichi kama matunda na karanga.
Kwa haya na mengine mengi usikose kufuatilia gazeti la TABIBU kila siku ya Alhamis

Kwa makala hizi na nyingine nyingi za kuelimisha kuhusu Afya, hakikisha hukosi kopi ya gazeti lako la TABIBU kila wiki siku ya Alhamis.

No comments:

Post a Comment