Tabibu Tv

Tabibu Tv

EBOLA BBC NEWS

Thursday, August 7, 2014

Fahamu ubora wa mafuta ya samaki katika ubongo


Chicago, Marekani


Tafiti zinasema kuwa mafuta ya samaki aina ya Omega-3 yanaweza kusaidia ubongo kutokana na matatizo yanayosababishwa na pombe kwa asilimia 90.
Watafiti wamegundua kwamba seli za ubongo zilizohusishwa na kiasi kikubwa cha pombe ziliweza kulindwa zisiharibike na hatimaye kufa kwa mkusanyiko unaopatikana katika mafuta ya samaki.
“Mafuta ya samaki yana uwezo wa kusaidia kuutunza uwezo wa ubongo katika matumizi mabaya kabisa ya pombe,” alisema mtafiti Michael Collins kutoka Shule ya Madawa ya Chuo Kikuu cha Loyola, Chicago Marekani.
Katika utafiti huo, Collins na wenzake waliweka ubongo wa panya katika kiwango cha pombe kinachozidi mara nne ya kiwango kinachoruhusiwa kisheria kwa waendesha magari, kiasi cha pombe ambacho huwa kinaonekana kwa wanywaji pombe waliokubuhu.


Tabia za ubongo huo ziliweza kulinganishwa na tabia za mkusanyiko huo huo wa ubongo uliowekwa pamoja na omega-3 “docosahexaenoic acid” (DHA) kutoka katika mafuta ya samaki.
Aidha, watafiti wamegundua kulikuwa na asilimia 90 ya upungufu ya ‘neuro-inflammation’ na kifo cha nuroni katika seli za ubongo zilizowekwa kwenye pombe na (DHA) kuliko zile seli zilizowekwa kwenye pombe peke yake.
“Pombe katika kiwango cha kawaida inaharibu seli na hivyo kuzifanya kuwa sugu na kuendana na matatizo makubwa yanayoweza kusababisha mzio. Lakini kiasi kikubwa cha pombe kinaharibu zaidi seli na kupelekea kuua seli na kusababisha ‘neuro-inflammation’,” alisema Collins.
Kulingana na watafiti, wanasema kuwa, haina maana kwamba watu watumie mafuta ya samaki halafu baada ya hapo waendelee kutumia pombe vibaya kwani hakuna manufaa watapata kwa njia hiyo.

Kwa habari kama hizi na nyingine nyingi hakikisha unapata nakala ya gazeti lako la TABIBU kila siku ya Alhamisi kwa shilingi 500/= tu

No comments:

Post a Comment