Tabibu Tv

Tabibu Tv

EBOLA BBC NEWS

Thursday, August 28, 2014

Kokwa la embe huweza kuondoa maumivu wakati wa tendo la ndoa


Dk Mandai
Maumivu wakati wa tendo la ndoa huwakabili baadhi ya watu na kusababisha walichukie au kukosa hamu ya kufanya tendo hilo.

Mara nyingi maumivu yanayotokea mwanzoni wakati wa tendo la ndoa halafu yanapotea baadaye, hali hii husababishwa na upungufu wa ute unaoilainisha njia ya uzazi na mara nyingi hutokana na maandalizi hafifu wakati wa tendo husika.

Wakati mwingine hali hii hutokea baada ya mwanamke kumeza dawa zinazohusisha majimaji ukeni kama vile dawa za kuzuia uzio na nyinginezo.

Adha, tatizo la maumivu wakati wa tendo la ndoa huweza kusababishwa na athari za kisaikolojia anazokuwa nazo mwanamke. Mfano kama mwanamke aliwahi kubakwa au kufanyiwa vitendo viovu mara nyingi mwanamke wa aina hii huweza kuwa na hali ya kutohisi hamu ya tendo la ndoa.

Wanawake wenye uwezekano wa kukumbwa na tatizo hili.
·      Niwale ambao muda wao wa kupata hedhi umekoma, hii ni kwa sababu baadhi ya vichocheo (homoni) vinavyochochea kutolewa kwa majimaji ili kulainisha njia ya uzazi hupungua kwenye damu, na wengine ni wale wenye matatizo ya maambukizi ya magonjwa katika viungo vyao vya uzazi hususani magonjwa ya zinaa.

·      Maambukizi kwenye njia ya mkojo hasa kwenye kibofu cha mkojo huleta maumivu wakati wa tendo la ndoa.



·      Wanawake wenye matatizo sugu ya kukosa choo wao wanauwezekano mkubwa wa kupata maumivu haya.

·      Endapo mwanamke atafanya tendo la ndoa kipindi kifupi mara baada ya kujifungua huweza kupata maumivu wakati wa tendo hilo. Mwanamke anapo jifungua viungo vyake vya uzazi huchukua muda mrefu hadi kurudi katika hali yake ya kawaida, hivyo basi anaposhiriki tendo la ndoa muda mfupi baada ya kujifungua atajisikia maumivu. Pia tatizo hili huwapata wanawake waliojifungua kwa kuongezwa njia ya uzazi.

 Maumivu kwa wanaume
Wanaume huweza kupatwa maumivu ya aina hii wakati wa tendo lenyewe au wakati wa kutoa mbegu. Pia maumivu haya husababishwa na maambukizi au vidonda kwenye ‘gland,’ ambayo huruhusu mbegu kutoka ‘prostate grand.’

Maumivu kwa wanaume pia husababishwa na maambukizi kwenye ngozi inayofunika uume na magonjwa ya malengelenge na baadhi ya magonjwa ya zinaa mara nyingi maambukizi haya husababishwa hata wakati wa kusimama. Hizo ni baadhi ya sababu, ambazo mara kwa mara husababisha tatizo hili.

Athari
Ni jambo la muhimu kwenda hospitali unapokuwa na tatizo hili kuliko kukaa kimya, jitahidi kumuelezea namna maumivu hayo yanavyokutokea. Mfano utapaswa kumueleleza daktari maumivu unayoyapata yana muda gani na hutokea baada ya tendo lenyewe au ni tofauti. Hivyo daktari atafahamu ni dawa gani akupatie.

Magonjwa ya zinaa yanachangia tatizo hili, hivyo ni vyema kwenda na mwenza wako mkachunguzwe na kutibiwa wote. 

Tiba hufanyika kwa kutegemea sababu iliyosababishwa na kumuona mtaalamu wa matatizo ya kisaikolojia kwa msaada zaidi, wale wenye tatizo la kisaikolojia wanashauriwa kumuona daktari wa matatizo ya kisaikolojia kwa msaada zaidi.

Kinga
·      Ni muhimu kuzingatia usafi kwani hupunguza uwezekano wa kupata baadhi ya maambukizo.

·      Kila mtu anatakiwa kumuandaa mwenzake wakati wa tendo hili ili kusaidia majimaji ya kulainisha njia ya uzazi yatoke ya kutosha
·      Wale wenye njia kavu zaidi mafuta maalumu ya kulainisha hutumika, isipokuwa hakikisha hautumie Vaseline au mafuta mengine ya mgando kwani yanaweza kurahisisha kupata maambukizo ya magonjwa.

·      Kwa wanawake hakikisha haushiriki tendo la ndoa mara baada ya kujifungua subiri angalau baada ya wiki sita.

Tiba
Chukua kokwa la embe ponda ponda kausha au twanga, kisha utapata unga wake ambao utatumia katika uji mwepesi 1x3 kwa muda wa siku 14.


Makala nyingi kama hizi unaweza kukutana nazo kupitia gazeti la TABIBU kila siku ya Alhamis kwa shilingi 500/=  tu.

Wednesday, August 27, 2014

Matatizo ya mkojo mchafu UTI




Dk Mandai
Mkojo mchafu (UTI) ni matatizo katika njia ya mkojo ambayo huchangiwa na maradhi na matatizo ya aina mbalimbali. Matatizo ya UTI husababishwa na vimelea (bacteria) ambavyo huingia katika njia ya mkojo.

Ugonjwa huu huweza kumpata mtu yeyote pasipo kujali ni mwanaume au mwanamke. Hata hivyo, mwanaume huweza kuhisi dalili za UTI mapema zaidi kuliko wanawake hii ni kutokana na tofauti za kimaumbile.

Wanawake kwa upande wao huathiriwa na UTI hasa kutokana na mfumo mzima wa maungo yao hasa ya mfumo wa mkojo kuwa na urahisi wa kuingiliwa na bacteria. Mathalani, mrija wa mkojo yaani urethra ya mwanamke ni fupi sana ukiliganisha na ya mwanaume na hivyo vijidudu au bakteria hupata urahisi wa kuingia ndani.

Chanzo cha UTI
Tatizo hili husababishwa na vyanzo mbalimbali, lakini zaidi maambukizi yanayosababisha tatizo hili ni bacteria au virus. Bakteria wanaosababisha UTI ni ‘e.coli’ na vijidudu vingine vya magonjwa ya zinaa mfano (klamidia) na vijidudu vya kisonono.

Virusi ambavyo husababisha tatizo hili ni kama vile ‘herpes simplex’ na ‘cytomegalo virus,’ sababu nyingine ni kuumia njia ya mkojo au kuwekewa mrija wa mkojo. Kemikali ni kama vile dawa za kuua mbegu za kiume au dawa za kupaka ukeni.
Kushiriki ngono na wanawake au wanaume wengi kwa upande wa wanawake pia ni mojawapo ya chanzo cha tatizo kwa kiasi kikubwa.

Wengine wanaopatwa zaidi na tatizo hili ni wale wenye tabia ya kufanya ngono au 
 kuwaingilia wengine kinyume na maumbile.

Dalili za UTI
Dalili zinazotofautiana kati ya mwanaume na mwanamke, mwanaume mwenye tatizo hili anaweza kukojoa mkojo wa njano sana kila wakati na unakuwa na harufu mbaya hata ukinywa maji mengi na wakati mwingine mkojo huambatana na damu.
Mwanaume anaweza kutokwa na manii au shahawa kwenye mkojo au anapojikamua haja kubwa, huhisi muwasho katika njia ya mkojo na ukiminya uume unahisi unauma na wakati mwingine unakuwa umevimba.

Uume ulegea au unaposimama huuma, vilevile hupata maumivu unapotoa manii wakati wa tendo, lakini manii huweza kuambatana na damu. 

Athari kubwa kwa wanaume ni kupungua nguvu za kiume na kuziba njia ya mkojo, Kwa wanawake hushambuliwa na maumivu ya tumbo chini ya kitovu, maumivu na moto wakati wa kukojoa, homa za mara kwa mara na kutetemeka, wakati mwingine unaweza kuhisi malaria au taifodi, pia kila mtu mwenye UTI huisi kukojoa mara kwa mara ,pamoja na nyonga zote huuma na hutokwa na uchafu ukeni unaoambatana na muwasho.  

Hata hivyo, ulaji wa tunda la tikiti maji kwa wingi huweza kusaidia sana kusafisha njia ya mkojo na kukusaidia kuondokana na tatizo hili la UTI. 

Kwa makala nyingine nyingi za afya hakikisha hukosi gazeti lako la TABIBU kila siku ya Alhamisi kwa shilingi 500/= tu.
 
Makala hii imeandaliwa na kuletwa kwenu na Mandai Harbalist Clinic, Kituo cha tiba asilia ya magonjwa sugu kilichopom jijini Dar es Salaam maeneo ya Mongolandege, Ukonga Mombasa. Au unaweza kuwasiliana nao kwa namba za simu; 0653 163 838 / 0752 163 838

Ona jinsi mzee huyu anavyoteswa na maradhi ya kibofu

Na Kenneth Maganga
Kushoto ni mwandishi wa TABIBU  akizungumza na Mzee Maulid alipomtembelea nyumbani kwake Mbagala Kongoe (Picha na mwandishi wetu)
  • ·      Kwa sasa anakojoa kupitia mirija

  • ·      Awaomba Watanzania kumsaidia na ikiwezekana aonane na JK


Mzee Maulid Kakonda mkazi wa Mbagala Kokongoe jijini Dar es Salaam amekuwa akiteseka na maradhi ya kibofu cha mkojo tangu mwaka 2012 na kupelekea kuishi na maumivu makali katika maisha yake tangu kukubwa na maradhi hayo.

Akizungumza na TABIBU hivi karibuni, Mzee Maulid anasema kuwa maradhi hayo yalianza kumsumbua mwaka 2012, ambapo alijikuta akianza kupata haja ndogo kidogo sana (mkojo), pamoja na maumivu makali na baadaye alishindwa kabisa kupata mkojo.

“Kwenye siku mbili tatu niliona mkojo unatoka kidogo sana na baadaye ukabana zaidi na kuacha kabisa kutoka,” alisema mzee Maulid.

Baada ya hali hiyo mzee Maulid anasema alilazimika kwenda Hospitali ya Taifa Muhimbili, ambapo madaktari waligundua alikuwa anasumbuliwa na tatizo la uvimbe kwenye kibofu na kupelekea kufanyiwa upasuaji na kuwekewa mirija miwili ambayo ndio inamsadia katika kutoa haja ndogo kwa sasa.

Kutokana na hali hiyo mzee huyo anasema kwa sasa kila baada ya wiki mbili huwa anakwenda hospitali kubadilisha mirija, ambapo anasema mara nyingi anapobadilishwa mirija hiyo hupatwa na maumivu makali ambayo mara nyingi humsababishia homa kali.

Mzee Maulid, anasema tangu alipoanza kusumbuliwa na maradhi hayo amekuwa akipatiwa matibabu bure, baada ya kupata msamaha wa matibabu, ambao aliupata kutokana na juhudi za Serikali yake ya mtaa, lakini kwa sasa anasema muda wa msamaha huo umekwisha, hivyo anahitajika kutoa pesa ili kuweza kuendelea na matibabu zaidi hususani upasuaji mwingine wa pili.

Hapo awali kabla ya maradhi hayo mzee Maulid, anasema alikuwa akipata ridhiki kupitia kuchukua magazeti yaliyokwisha somwa katika ofisi mbalimbali, kisha kuyauza kwa wamiliki wa maduka, ambayo hutumika kufungia bidhaa mbalimbali. Lakini kwa sasa kutokana na maradhi yake hayo amekuwa akishindwa kufanya shughuli hizo hivyo kupelekea maisha ya familia yake yenye jumla ya watu 6 kuwa katika hali ngumu zaidi.

“Maisha yangu bado ni ya shida kwa sasa, kwa sababu hapa nilipo bado sijajua lini nitapata uzima, lakini naamini kwa uwezo wa mwenyezi Mungu madaktari watanifanyia huduma,” alisema Mzee Maulid.

Mbali na maradhi hayo mzee Maulid pia anatatizo la ulemavu, ambapo anasema ulemavu huo aliupata kupitia kwa waganga wa jadi, baada ya kukupwa na ganzi mwilini, tatizo lililompelekea kwenda kwa waganga wa jadi ambako alikuwa akipatiwa matibabu ya tatizo hilo kwa njia ya kuchua.

“Mimi nilizaliwa mzima kabisa, lakini matatizo haya ya miguu yametokana na waganga wa jadi, ambao walikuwa wakinichua sana pindi nilipokuwa nikisumbuliwa na ganzi mwilini, lakini kumbe walikuwa wananichua kwa nguvu nyingi sana na mwishowe nilijikuta nikiwa katika hali hii unayoniona nayo,” alisema Mzee Maulid.  

Pamoja na hayo, mzee huyo amewaomba Watanzani kumsaidia ili aweze kuendelea na matibabu yake, lakini pia ameomba kusaidiwa kutokana na hali ngumu ya maisha yake anayoipitia kwa sasa yeye pamoja na familia yake.

Miujuza ya kitunguu maji


Dk Edger Kapagi
Kitunguu ni mojawapo ya mimea ambayo wanadamu wamekuwa wakikuza kwa muda mrefu sana. Asili yake ni Persia. Kitunguu kimelimwa katika bonde la Mto Nile miaka 6000 kabla ya kristo.
Kwa sasa kinalimwa Ulaya, Misri, America, India, China, Japan, Malaysia na Africa mashariki na kati nk.
Katika nchi nyingi kitunguu hakiwezi kukosekana jikoni. Bila shaka, kinatumiwa kwa njia mbalimbali kama vile vyakula tofauti, na dawa. Pia kinaweza kufanya utokwe machozi. Hali kadhalika kitunguu ni mojawapo ya mimea inayochanua maua maridadi.
Hata hivyo, watu wengi ulimwenguni hutumia kitunguu kilicho na shina lenye tabaka za mviringo ambalo hukua chini ya ardhi. Aidha, vitunguu huwa na rangi tofauti, tofauti kama vile nyeupe, manjano, kahawia, kijani, nyekundu na zambarau.
Unaweza kula vitunguu vikiwa vibichi au vikiwa vimepikwa. Pia unaweza kula achali ya vitunguu, vitunguu vilivyokaushwa, vilivyosagwa na vilivyokatwakatwa.
Ni wazi kuwa kitunguu ni mmea wa ajabu, hata kama kitafanya utokwe na machozi. vitunguu huboresha sana afya ya watu, kwani huwa na protini, mafuta, nyuzinyuzi, madini, wanga, kalisiumu, fosforasi, chuma, carotene, ‘thiamine B1 niacin B3, riboflavin B2, sulphur, asidi askobiki au vitamin C na K.

Hata hivyo, kwa miaka mingi vitunguu vimetumiwa hasa kwa matibabu. Hata leo vinatumika kutibu magonjwa mbalimbali kama vile mafua, kuvimba koo, utando mgumu wa mafuta katika mishipa ya damu, ugonjwa wa moyo, kisukari, pumu, kuzuia lehemu (cholesterol), uvimbe, kuganda kwa damu ndani ya mishipa, tambazi, kusinyaa kwa ini (cirrhosis), vidonda, kuharisha, kupunguza ‘uric acid’, ‘hemorrhoids,’ kikohozi, ‘bronchitis, ’freckles,’ kipindupindu, kuuma sikio, kukuza nywele, hufaa kwa wenye matatizo ya nguvu za uzazi. (hapa hakikisha unatibu kilichosababisha kupungua kwa nguvu za uzazi).
Magonjwa mengine ni matatizo ya meno, matatizo ya ini, matatizo ya ngozi, maumivu ya viungo na ‘arthritis’ ikichanganywa na mafuta ya haradali, maumivu ya kichwa, majipu, matatizo ya tumbo na pia vitunguu hutumiwa katika dawa za kusafisha vidonda na mengineyo mengi. Kitunguu kinapendwa sana tutumie kwa ajili ya afya zetu.
Ukifanya jitihada za kututembelea ofisini utajua tunatibu maradhi mengine pia ikiwamo homa ya matumbo (Typhoid), Malaria, michirizi inayosababishwa na ujauzito( Stretch Marks in Pregnancy), mkanda wa Jeshi (Herper Zosters), Magonjwa ya ngozi, tumbo, kuimarisha kinga ya mwili, kuondoa gesi tumboni, kupunguza makali ya saratani, kisukari, BP ya kupanda. Mengine ni pamoja na maumivu makali wakati wa hedhi (Dysmenorrhea), kutoka damu nyingi wakati wa hedhi (Menorrhagia), kukawia kuingia hedhini (Amenorrhea), matatizo ya kukoma kwa hedhi (Menopause), kulegea kwa uzazi (vagina discharge), miguu kuwaka moto, vidonda vya tumbo, kufunga kuharisha, matatizo ya uvimbe wa kizazi na mengine mengi ambayo si rahisi kuyaorodhesha isipokuwa baadhi.
Na kadri mgonjwa anapofika na kujieleza, ndivyo tunavyotambua Tatizo analokuwa nalo na anahitaji tiba ipi. 
Kwa makala nyingi na nzuri kama hizi hakikisha hupitwi na gazeti la TABIBU kila siku ya Alhamisi kwa shilingi 500/= tu.
 


Mazingira Natural Products
Mbeya
Simu; +255 754 807401, +255 719 564276
Barua pepe; mnp.kaka@gmail.com


Chungwa: tiba ya kuzibua mirija


Habari mpenzi msomaji wa blog ya gazeti la TABIBU, ni matumaini yangu mzima wa afya. Karibu tena katika safu hii kutoka Miracle Food, ambayo hupatikana kila siku ya Alhamisi katika gazeti la TABIBU, kama ilivyokawaida wajibu wetu ni kukupa elimu ya afya na vyakula mbalimbali. Leo tumekuandalia chungwa kama tiba ya magonjwa mbalimbali lakini hasa kuzibua mirija ya uzazi kwa wanawake.

Pamoja na uwepo wa maradhi mengi ya mfumo wa uzazi wa akina mama kama kutokwa na damu nyingi au kidogo wakati wa hedhi, maumivu wakati wa hedhi au wakati wa tendo, tatizo la mayai kutopevuka kwa wakati nk. Lakini hasa tutakachokiangalia leo ni kuziba kwa mirija ya uzazi.

Chungwa ni tunda linalostawi ulimwenguni kote, lakini haswa lilianzia kusini mwa bara la Asia, huku likilimwa sana huko nchini China.

Miaka ya nyuma sana mnamo 2500 BC (kabla ya kristo) chungwa limekuwa likiitwa tufaa la kichina, baada ya hapo watu wakalieneza Uingereza na Marekani katika miaka ya 1500. Hata hivyo mnamo mwaka 1897 tunda hili likatambulika ulimwenguni kote. Tunda hili huweza kuliwa likiwa katika hali ya uhalisia (fresh) au kwa kutengeneza juisi.

Kwa kawaida chungwa limekuwa likisifika kwa uwingi wa vitami C, lakini kwa sasa imegundulika licha ya kuwa na vitamin C pia lina zaidi ya ‘phytochemicals’ 170, ambazo husaidia ufanyaji kazi wa vitamin mwilini. Ingawaje wataalam wanasema kuwa vitamin C inayopatika kwa ulaji wa chungwa inaweza kuwa na kiasi kikubwa zaidi ya kinachohitajika mwilini hivyo ni hatari, kwa hiyo huwa wanashauri ni vyema kupata vidonge vya vitamin hospitali.



Chungwa lina sehemu kuu tatu nazo ni
 Ganda (exocarp): hili eneo la nje kabisa ambalo lina mafuta ya muhimu yenye ‘flavonoids.’ Ganda la chungwa hutumika kulinda mfumo wa misuli na kuongeza hamu ya kula na kutuliza mishipa ya fahamu.

Ganda jeupe la ndani (mesocarp) : hili ni eneo la ndani ambalo huonekana baada ya chungwa kumenywa, ganda hili jeupe lina ‘pectin,’ ambayo ni aina ya nyuzinyuzi (fibre) zipatikazo kwenye mbogamboga. kazi yake ni kuzuia lehemu (cholesterol) na kansa, ni vyema kuthamini afya yako kwa kutolitupa ganda jeupe la chungwa ingawa halina ladha nzuri ya kukuvutia lakini ni vyema ule.

Endocarp: (Juicy Pulp): hili ni eneo la ndani ambalo ndio hutoa juisi, watu wengi hukimbilia hapa, limetengwa kwa vyumba vyumba vipatavyo 8 mpaka 12 ambamo kuna chembe (cell) ndogondogo zenye maji ya matunda (Juice). Mistari hii iliyotenganisha vyumba hivi, baada ya kuwa maji ya tunda yameshakamuliwa bado ina kiasi cha ‘pectin’ kama (fibre) nyuzinyuzi za

Aina nyingine za mbogamboga.
Tofauti ya tunda na (Juice) maji yake ni kwamba unapokunywa juisi unapata virutubisho sawa kwa njia rahisi, lakini ‘calcium’ na ‘fibre’ inakosekana ambayo hupatikana kwenye ulapo tunda lenyewe. Wakati wa utengenezaji au uandaaji wa juisi ya chungwa vitamin C hupotea kwa asilimia 10. Virutubisho vilivyobaki huwa kama vilivyo na haswa juisi ilitiwa ubaridi wa jokofu na hata kuganda ni nzuri zaidi.

Inaaminiwa kuwa kula machungwa manne kwa siku ni kinga sahihi kwa wale wanaohitaji kinga ya maambukizi ya magonjwa mbalimbali.

Mpenzi msomaji wa blog hii ya TABIBU hadi kufikia hapo ndio mwisho wa somo letu la machungwa kwa kutumia kama tiba ya kuzibua mirija ya uzazi na maradhi mengineyo, tukutane tena wiki ijayo katika mfululizo wa masomo mengine ndani ya gazeti la TABIBU kila siku ya Alhamisi kwa shilingi 500/= tu.

Kwa maelezo zaidi wasiliana na Miracle Food Clinic & Counseling kwa simu namba 0755 093 418, 0715 093 418 na 0688 063 418. Tupo Kariakoo mtaa wa msimbazi jengo la Klabu ya Simba ghorofa ya tatu. Karibuni