Tabibu Tv

Tabibu Tv

EBOLA BBC NEWS

Friday, December 19, 2014

Ndizi na faida zake kiafya

Na Zamda Haroun

Ndizi ni tunda muhimu Afrika Mashariki na katika nchi za joto na hasa katika visiwa vya Caribbean. Mmea wake huitwa mgomba katika nchi za Afrika Mashariki.
Tunda hili ambalo lina asili ya kusini mwa Asia huonekana na rangi nzuri na mara nyingi tumezoea kuliona shambani au maeneo ya sokoni na limeonekana kuwa na faida nyingi kiafya.

Miongoni mwa faida za tunda hili ni pamoja na kuboresha ngozi, hususani maganda yake ambapo yanaaminika kusaidia kuimarisha ngozi pale yanaposagwa vizuri na kuchanganywa na matunda mengine kama parachichi. Mchanganyiko huo kwa pamoja husaidia kulainisha ngozi na kuifanya kuonekana vizuri na yenye kung’aa.
Aidha, ndani ya ndizi kuna vitamin B6 na vitamini C, lakini vitamini B6 ndio hupatikana kwa kiwango kikubwa zaidi ndani ya tunda hilo kuliko vitamini C ambayo ni kidogo.
Hali kadhalika, ndizi husaidi kuongeza idadi ya chembe chembe nyeupe za damu hivyo huweza kumsaidia mtu katika uboreshaji wa kinga mwilini.
Faida nyingine za ndizi ni pamoja na kuongeza nguvu mwilini. Hii ni kwa sababu tunda hilo huwa na sukari ijulikanayo kama ‘glucose,’ ambayo husaidia sana kuongeza nguvu mwilini, ingawaje sukari hiyo huhitajika katika kiasi maalum mwilini.
Pamoja na hayo, ndizi pia huweza kusaidia sana kukukinga na kupata vidonda vya tumbo kutokana na ‘compounds,’ mbalimbali zilizomo ndani ya tunda hilo. ‘Compounds,’ hizo ambazo hupatikana kwenye ndizi hujenga tabaka nene kwenye kuta za tumbo ambazo husaidia tumbo kuzuia kuathirika na tindikali ijulikanayo kama ‘hydrochloric acid’.
Aidha, ndizi zina ‘enzyme’ inayojulikana kama protease inhibitor,’ ambayo huzuia bakteria wasababishao vidonda vya tumbo.

Hizo ni baadhi ya faida chache tu za ndizi, ingawaje zipo nyingi zaidi, lakini kwa leo tuhitimishie hapo. Hakikisha unadumisha kutumia tunda hili mara kwa mara ili uweze kuimarisha afya yako zaidi.

No comments:

Post a Comment